Skip to content

Makocha Wanaolipwa Mamilioni EPL: Arteta Aongoza, Alonso Aingia Top 3

SokaNews
Updated: Published: Jumatano, 3 Juni 2026 · 5 min read
premierleague makocha mishahara arsenal chelsea tottenhamhotspur
Makocha Wanaolipwa Mamilioni EPL: Arteta Aongoza, Alonso Aingia Top 3

Makocha Wanaolipwa Mamilioni EPL: Arteta Aongoza, Alonso Aingia Top 3

Premier League si ligi ya mishahara mikubwa kwa wachezaji pekee. Hata makocha nao wanachukua fedha ndefu, na orodha mpya ya waliolipwa zaidi imeonyesha wazi jinsi vilabu vya England vilivyo tayari kufungua mifuko ili kupata watu wanaoaminiwa kuleta matokeo.

Kwa kuondoka kwa majina makubwa kama Pep Guardiola na Arne Slot, sura mpya zimeingia kwenye orodha hii, ikiwemo kocha mmoja kutoka klabu iliyopanda daraja. Hapa chini ni makocha saba wanaolipwa zaidi kwenye ligi kuu ya England kwa sasa.

7. David Moyes – Everton (£5m kwa mwaka)

David Moyes alirejea Everton katika kipindi ambacho klabu hiyo ilikuwa ikihangaika kupambana na hatari ya kushuka daraja. Inaelezwa alijadiliana mshahara mzito ili kurudi kuinoa timu ya Merseyside, na mpaka sasa ameanza kuhalalisha dau hilo.

Ameisaidia Everton kujiondoa kwenye eneo la hatari na kufika salama katikati ya msimamo, lakini sasa swali kubwa ni kama ataweza kuchukua hatua inayofuata na kuisukuma timu kuwa na ushindani zaidi.

7. Kieran McKenna – Ipswich Town (£5m kwa mwaka)

McKenna alipoiongoza Ipswich kupata promotion ya kwenda Premier League, vilabu kadhaa vilianza kumwazia. Ili kumuweka Portman Road, uongozi wa Ipswich uliamua kumjaza mfuko zaidi, na mshahara wake ukaripotiwa kupanda mara tatu hadi takriban pauni milioni 5 kwa mwaka.

Hiyo inamfanya awe miongoni mwa makocha wanaolipwa vizuri zaidi kwenye ligi, hatua kubwa kwa kocha aliyekuwa akivutia sana hata kabla ya kupanda daraja. Mashabiki wa Ipswich wanaweza kusema ni fedha zinazostahili, hasa kwa mtu aliyewaongoza kupanda daraja mara tatu katika misimu yake minne kamili.

Kazi yake sasa ni kuhakikisha Suffolk club inabaki EPL kwa muda mrefu.

5. Eddie Howe – Newcastle United (£6m kwa mwaka)

Eddie Howe aliipokea Newcastle wakati ikiwa kwenye vita ya kushuka daraja, lakini amefanikiwa kuibadilisha timu hiyo kuwa nguvu ya kuogopwa, ikiwemo kuifanya iwe miongoni mwa timu zinazowania nafasi za Champions League kwa utaratibu.

Zaidi ya hilo, ameipa klabu kombe la kwanza baada ya miaka mingi, jambo ambalo kwa mashabiki wengi linatosha kuhalalisha mshahara wake wa pauni milioni 6 kwa mwaka.

Hata hivyo, kwa mara ya kwanza, kuna maswali mazito kuhusu kama anaweza kuipeleka Newcastle hatua nyingine zaidi. Msimu dhaifu wa ligi, uliosindikizwa na vipigo viwili dhidi ya wapinzani wao waliopanda daraja Sunderland pamoja na aibu dhidi ya Barcelona, umeacha maswali mengi kabla ya majira ya joto.

Kama viongozi wa Newcastle wako serious kutaka kuingia daraja la juu la matajiri wa EPL, Howe anaweza pia kujikuta kwenye shinikizo kubwa.

4. Unai Emery – Aston Villa (£8m kwa mwaka)

Ukilinganisha hali ya Aston Villa alipowasili na walipo sasa, ni wazi Unai Emery analipwa kwa haki kabisa. Alipochukua timu hiyo Oktoba 2022, Villa walikuwa wanaonekana kama waathirika wa kushuka daraja. Leo hii, wamekuwa timu inayojipigania nafasi za Champions League kwa utaratibu.

Emery pia ameiletea klabu mataji, jambo linaloongeza uzito wa mchango wake. Ingawa kanuni za PSR zimeweka kikomo fulani kwa uwezo wa Villa kupiga hatua kubwa zaidi kifedha, ni rahisi kuona kwamba bila kocha huyu, wangeshuka kiwango.

3. Xabi Alonso – Chelsea (£11.5m kwa mwaka)

Liverpool kuchelewa kuchukua hatua kulimpa Chelsea nafasi ya kuminyakua Xabi Alonso, ambaye amekubali kujiunga na The Blues badala ya kurejea Anfield.

Taarifa za kumuita “manager” badala ya “head coach” zilionekana kama ishara ya mabadiliko ya fikra ndani ya uongozi wa Chelsea, na inaelezwa kuwa dau lake ni kubwa sana. Ripoti zinaonyesha analipwa pauni milioni 11.5 kwa mwaka, kiwango kinachomweka nafasi ya tatu kwenye orodha ya makocha wanaolipwa zaidi Premier League.

2. Roberto De Zerbi – Tottenham Hotspur (£12m kwa mwaka)

Tottenham waliingia kwenye mazungumzo na Roberto De Zerbi wakiwa katika mazingira magumu ya kujadiliana, lakini hata hivyo mkataba uliotolewa unaonekana kuwa wa gharama kubwa.

De Zerbi analipwa pauni milioni 12 kwa mwaka, na kwa upande wa Spurs wanaweza kusema ni fedha zilizoelekezwa kwa mtu aliyesaidia kuisukuma timu kubaki juu. Kwa sasa, watauchukulia kama uwekezaji unaostahili.

Hata hivyo, ana mkataba wa miaka mitano na si kocha anayejulikana kwa kukaa sehemu moja kwa muda mrefu. Hilo linaweza kuwa tatizo baadaye ikiwa itabidi atimuliwe, kwani gharama ya uamuzi huo inaweza kuwa kubwa sana.

1. Mikel Arteta – Arsenal (£15m kwa mwaka)

Kwa kuondoka kwa Pep Guardiola na mshahara wake wa pauni milioni 20, Mikel Arteta amepanda hadi kileleni mwa orodha hii.

Maswali ya muda mrefu kuhusu kama ataipa Arsenal mataji makubwa yameanza kupata majibu. Mkataba wake wa sasa unaelezwa kuisha mwaka ujao, na kuna uwezekano mkubwa wa kuongezewa mkataba mpya wenye mshahara mkubwa zaidi.

Na kwa kweli, itakuwa ni malipo ya kustahili kwa kazi aliyofanya tangu achukue timu Desemba 2019. Alipoingia, Arsenal ilikuwa timu yenye nidhamu duni na iliyomaliza nafasi ya tano chini ya Unai Emery. Leo, Arteta amebadili kabisa utamaduni wa klabu hiyo.

Ameondoa pia wachezaji wenye utata kama Pierre-Emerick Aubameyang, na kujenga safu ya ulinzi ambayo huenda ikawa miongoni mwa imara zaidi duniani.

Orodha hii inaonyesha kitu kimoja tu: Premier League inaendelea kuwa soko kubwa la fedha, na makocha wanaofanikiwa hawachelewi kufaidika.